JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA

Majukumu

Majukumu ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa yameainishwa katika Sheria ya Vyama vya Siasa nayo ni haya yafuatayo:-

  1. Kusajili na kufuatilia utendaji wa vyama vya siasa kwa mujibu wa Sheria;
  2. Kuratibu shughuli za Baraza la Vyama vya Siasa;
  3. Kufuatilia mapato na matumizi ya vyama vya siasa;
  4. Kugawa na kufuatilia matumizi ya fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa vyenye sifa;
  5. Kutoa elimu ya uraia kuhusu sheria zinazosimamiwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na mfumo wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa;
  6. Kuratibu elimu ya uraia inayotolewa kwa vyama vya siasa;
  7. Kufanya utafiti kuhusu masuala ya siasa na demokrasia ya vyama vingi;
  8. Kuwa kiungo kati ya Serikali na vyama vya siasa; na
  9. Kuishauri Serikali kuhusu masuala yanayohusu vyama vya siasa.
  10. Pamoja na majukumu yaliyoainishwa hapo juu, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ina jukumu la kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi sura ya 278